MATCHDAY: KENGOLD 🆚 SIMBA SAA 10:00

Kikosi cha Simba leo saa 10 jioni kitashuka uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora kumenyana na KenGold katika mchezo wa ligi kuu, mzunguuko wa 29
Ni katika moja ya mechi nane zitakazopigwa katika viwanja mbalimbali katika muda mmoja, saa 10 jioni
Simba itaingia katika mchezo huo ikiwa na malengo ya kuzisaka alama tatu muhimu ili kuendelea kusalia katika mbio za ubingwa
Wapinzani wao KenGold itakuwa mechi ya kukamilisha ratiba kwa upande wao kwani tayari wameshashuka daraja
Pengine inaweza kuwa mechi nzuri kwa Simba sio kusaka alama tatu tu, pia kujaribu kujiongezea mtaji wa mabao
Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davids amesema wamekuwa na maandalizi mazuri kuelekea mchezo huo na hawatawadharau wapinzani wao kwani ni timu ambayo haina cha kupoteza
Kikosi cha Simba kilitua mkoani Tabora mapema jana na jioni timu ikapata nafasi ya kukamilisha maandalizi yake katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi
Usikose kuitazama mechi hii live bure hapa hapa mwanajamii unachotakiwa kufanya ni kushea habari hii kwenye magroup yako ya whatsapp na facebook pia link ya mechi itawekwa kabla ya mechi kuanza
Â
