CHE MALONE, MUSA CAMARA NA WENGINE KUPEWA THANK YOU MUDA SI MREFU

CHE MALONE, MUSA CAMARA NA WENGINE KUPEWA THANK YOU MUDA SI MREFU
Mpaka sasa kiungo Fabrice Ngoma tayari amewaaga mashabiki wa Simba baada ya mkataba wake kumalizika
Ngoma hakusubiri kupewa Thank You baada ya mazungumzo ya kuhuisha mkataba wake kugonga mwamba
Mlinda lango Aishi Manula nae ni mchezaji wa pili kuondoka Simba baada ya mkataba wake kumalizika
Manula tayari amesaini kuitumikia Azam Fc kinachosubiriwa ni klabu hiyo kumtambulisha
Ukiachana na wachezaji hao, kuna orodha ya wachezaji wengine ambalo panga la Simba huenda ‘likapita nao’
Wachezaji ambao walikuwa nafasi finyu katika kikosi cha kwanza kama beki Hussein Kazi, mlinda lango Hussein Abel ni miongoni mwa wachezaji hao
Lakini pia wapo wachezaji ambao licha ya kutopata nafasi mara kwa mara, wanaweza kuhitajika baadae, hao huenda wakatolewa kwa mkopo
Hapa wachezaji kama Edwin Balua, Ladark Chasambi, Omary Omary, Ali Salim na Valentino Mashaka ni miongoni mwao
Pia ipo orodha ya wachezaji ambao wanaweza kuondoka kutokana na mahitaji ya maboresho ya kiufundi licha ya kuwa walitumika katika kikosi cha kwanza
Beki Che Malone Fondoh amemaliza mkataba lakini huenda asiongezewe mkataba mwingine Simba ikiwekeza nguvu kusaka beki mwingine wa kati huku kiungo Augustine Okejepha akiwekwa sokoni kama ilivyo kwa Steven Mukwala ambaye taarifa za ndani zimedokeza kuwa Simba imepokea ofa kwa ajili ya mchezaji huyo raia wa Uganda
Simba pia inatajwa kuwa katika mchakato wa kusajili magolikipa wawili mmoja wa ndani na mwingine wa kigeni, hiyo ikimaanisha huenda Moussa Camara nae akaachia nafasi yake
Mbivu na mbichi za usajili zitaanza kufahamika wiki ijayo kwani Simba itahitaji kukamilisha michakato yake yote ya maboresho kabla ya timu kuelekea pre-season
MIENDELEZO YA MUVI HIZI NA NYINGINE DOWNLOAD APP YETU
App bado hatujaiweka playstore hivo utaidownload kama APK
BONYEZA HAPA KUIDOWNLOAD APP ITAKAYOKUWEZESHA KUTAZAMA MUVI BURE
