ALI MAYAY NAYE ALALAMIKA KUHUSU KARIA KESI KUCHUKULIWA BMT

ALI MAYAY NAYE ALALAMIKA KUHUSU KARIA KESI KUCHUKULIWA BMT

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo Ali Mayay ni miongoni mwa wagombea waliojitosa kuwania kiti cha Urais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Leo ndio siku ya mwisho kwa wagombea waliochukua fomu kuzirejesha ambapo Mayay ni miongoni mwa waliorejesha fomu hizo licha ya kukumbana na changamoto ya kupata wadhamini

Rais anayetetea kiti chake Wallace Karia inaelezwa amechukua ‘Endorsement’ zote na hivyo kuwafanya wagombea wengine wakose na kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi, waliorejesha fomu bila ‘endorsement’ wataenguliwa kwa kukosa moja ya vigezo

Mayay amesema licha ya kukosa ‘endorsement’ amerejesha fomu ili kukamilisha hatua ya kwanza ya mchakato huo wa uchaguzi

Inaelezwa wagombea ambao wamekosa ‘endorsement’ wanakusudia kufungua malalamiko BMT kupinga kanuni hiyo inayowanyima haki ya kuwa wagombea

Kanuni wanayoilalamikia ni inayohusu mgombea kukosa sifa endapo atakosa walau wadhamini/wajumbe wa 5 kwa njia ya barua

Inaelezwa wajumbe wote 47 wamemdhamini mgombea anayetetea kiti chake, Karia

Add a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *